Breaking News

MPASUKO WANUKIA CHADEMA S'WANGA

M/kiti CDM Mkoa, Zeno Nkoswe
KUNA hatari ya kutokea kwa mvurugano ndani ya Chama Cha demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani Rukwa, baada ya kuibuka kwa kundi la watu wanaoulalamikia uongozi wa Chadema Sumbawanga mjini na ngazi ya mkoa kwamba unaanda mazingira ya kuwanyima haki baadhi ya watia nia ya kugombea ubunge katika jimbo la Suimbawanga mjini huku wakionyesha dhairi kumkumbatia mtia nia mmoja mwenye mwenye uwezo wa kiuchumi.



 Mazingira hayo yanatajwa kwamba yanaweza kukisambaratisha Chama hicho, ambacho kimeanza kukubalika na kujizolea viti kadhaa katika uchaguzi wa Serikali za mitaa uliopita, hali ambayo imeonyesha kuwa ni tishio kwa CCM katika uchuguzi mkuu ujao wa Rais, Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari jana mmoja wa wanachama wa Chadema, Datus Sikazwe alisema kuwa baadhi ya viongozi (majina yanahifadhi) wenye uwezo wa kufanya maamuzi ndani ya Chadema wamekuwa wakimkumbatia mgombea mmoja wenye uwezo wa kiuchumi na kumuandalia mazingira ya kumteua kuwa mgombea ubunge kupitia Chadema katika jimbo hilo, hali ambayo inaweza kusababisha mgogoro mkubwa na hatimaye kukisambaratisha chama hicho katika siku zijazo.

"Unajua kila mtia nia iwe Ubunge au Udiwani ana makundi yake, sasa haingii akilini kila katika mikutano ya Chadema, viongozi wanaambatana na mgombea mmoja (mwenye fedha)kisha wanampa fursa ya kupanda jukwaani na kumdani kuwa ndio mgombea ubunge wakati yeye ni mtia nia tu ya ubunge, kama walivyo watia nia wengine ambao hawataki kuambatana nao katika mikutano hiyo wala kuelezea kwamba kuna idadi kadhaa ya watia nia......maana yake ni kwamba huyu anandaliwa mazingira ya kuteuliwa kitu ambacho ni kibaya na kinaweza kutugawa na wenzetu wakapata mwanya wa kutushinda katika uchaguzi mkuu ujao" alisema.
 

Aidha Blog ya Pembezonikabisa imebaini kuwa kundi la mmoja wa watia nia ya ubunge, Emmanuel Msengezi ambaye ni kijana mzawa na msomi ndio limekuwa likilalamika kwamba uongozi wa Chadema unandaa mazingira ya kuteua jina la Sadriki Malila ambaye ni mfanyabiashara maarufu kwa jina la IKUWO amekuwa akishirikishwa katika kila kitu na uongozi huo hali ambayo inatafsiriwa kuwa ni kumuandaa kuwa mgombea ubunge wa jimbo hilo.
Taarifa zinaeleza kuwa wafuasi hao wa Msengezi wanadaiwa kupeleka malalamiko hayo kwa wazee wa Chadema wa Sumbawanga mjini wakiwataka kukaa na uongozi huo ili kuwasihi waache kutengeneza mazingira ya kuwakatisha tamaa watia nia wengine hali ambayo inaweza kusababisha kujitoa ili mtia nia huyo abaki peke yake na kuteuliwa kugombea ubunge.

Hata hivyo, Msengezi alipoulizwa kwa njia ya simu hakuwa tayari kuzungumzia lolote kuhusu sakata hilo kwa madai kwamba kwa sasa yupo safarini kikazi.

Mmoja wa Wazee hao,Norbert Yamsebo, ambaye aligombea ubunge mwaka 2010 na kuangushwa na Aeshi Hilaly, alikiri kukutana na mwenyekiti wa Chadema lakini hakuwa bayana kueleza kile walichokijadili lakini alidai kulikuwa na malalamiko mmoja wa watia nia ya ubunge.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Rukwa, Zeno Nkoswe licha kukiri kufanya mazingumzo na wazee ambao ulikuwa sehemu ya ujumbe kutoka kwa mmoja wa watia nia ya ubunge lakini alidai kwamba Chama hicho hakipo tayari kukumbatia watu ambao wanakiuka utaratibu tuliojiwekea.

"Kuna utaratibu tumeweka kwa watia nia ya ubunge na udiwani kwamba watakuwa wakishiriki kwenye shughuli zote za ujenzi wa Chama sasa kuna baadhi hawataki badala yake wanafanya kampeni nyakati za usiku......tena kampeni za ukabila sasa sisi katika chama kampeni za hivyo hazina nafasi" alisema Mwenyekiti huyo

Aliongeza kuwa Chadema ipo imara kwa sasa na wanajipanga kuweka watu ambao watakuwa sahihi kugombea ubunge ili waweze kufikia malengo yao ya kuchukua majimbo yote matano ya mkoa wa Rukwa.

Hata hivyo mmoja wa viongozi wa juu ambaye hakuwa tayari kutajwa jina lake alisema kuwa ni wazi Chadema tayari imemteua Ikuwo kugombea ubunge katika jimbo hilo kwa kuwa amekuwa na mchango mkubwa wa kifedha katika ujenzi wa Chama kuliko wagombea wengine ila kinachofanyika sasa ni utaratibu tu.

No comments