Breaking News

Shughuli za kiuchumi zachangia kuharibu mazingira ya Rukwa na Katavi.




Ongezeko kubwa la shughuli za kiuchumi katika mikoa ya Rukwa na Katavi, inatajwa ni moja ya changomoto kubwa katika uhifadhi na usmamizi wa mazingira katika mikoa hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Nchi , Ofisi  ya Makamu  wa Rais (Mazingira ) Januari Makamba,  Naibu Katibu Mkuu Ofisi  ya Makamu wa Rais (Mazingira ) , Mhandisi Ngosi Mwihava  alisem,a hayo jana wakati wa uzinduzi wa mradi wa Jumuiko la Pamoja , Suluhisho  la Pamoja (JUPASUPA)  ulifanyika mjini hapa.

Mradi huo  ni ushirikiano kati ya Serikali ya Uholanzi , Shirika  la Kimatiaifa  la Uhifadhi wa mazingira  la Uholanzi (WWF NL) , Shirika la Kimataifa  Kaengesa  Rukwa (KAESO).


Alisema kutokana na mikoa hiyo kuwa na fursa nyingi za kiuchumi, kasi ya ongezeko la watu wanaofanya shughuli hizo imekuwa kubwa hasa katika maeneo ya Kilimo, ufugaji, Uvuvi, uchimbaji wa Madini, uboreshaji wa miundombinu na uwekezaji mkubwa hali ambayo inahitaji uangalifu wa ziada katika kuhifadhi na usimamizi wa mazingira.

 Alisema uangalifu wa ziada unahitaji kwa kuwa watu  na mifugo ambayo  wote wanategemea mifumo ikilojia.

Alisema  hali ya uharibu wa mazingira ni kubwa ambapo kil mtanzania hutumia takribani  meta moja ya ujazo ya kuni au magogo kwa ajili ya  nishati  tu  ikiwa ni sawa na zaidi ya meta za ujazo milioni  50 kwa mwaka.

Aidha kasi  ya  uangamizaji misitu  nchini inakadiriwa  kufikia  ekari 372 , 000 kwa mwaka .

Mtendaji Mkuu wa KAESO , Ozem Chapita alisema kuwa  mradi huo utatekelezwa katika mikoa  miwili ya Rukwa na Katavi  lengo likiwa kuhakikisha  kunakuwa na usimamizi endelevu wa vyanzo vya maji , uhifadhi wa maliasili, uwekezaji rafiki wa mazingira  na kuongeza jitihada  za kukabiliana na mabadiliko  ya tabia nchi.
Alisema ili kuhakikisha  uendelevu wa mradi  huu hasa  katika utekelezaji katika ngazi  ya Taifa  asasi zingine zikiwemo  Haki Ardhi , Action Aid Tanzania  (AATZ)  na Shirikisho la timu  ya Wanasheria wa Mazingira Tanzania (LEAT) zitashiriki  katika mradi huu  kwa kusaidiana na Serikali  katika kuandaa  na kutekeleza  sera bora na mipango madhubuti  ya usimamizi wa ardhi , maliasili  na hifadhi ya mazingira katika  mikoa ya Rukwa na Katavi.

Mwakilishi wa Mkuu wa mkoa wa Rukwa , Albinus Mgonya alizitaka halmashauri zote  za mikoa  hiyo utendaj wake  uwe na lengo la  kutoa matokeo bora  zaidi ili kunusuru  rasilimali aslilia  ili kuinusuru  jamii  ili kufanikisha  mradi huo.

No comments