MKAZI WA MPANDA AENDA JELA KWA KUTAKA KUMBAKA MAMA YAKE MZAZI
Peti Siyame, Sumbawanga
MAHAKAMANI ya Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Rukwa imemuhukumu Ernest Fredrick (38), mkazi wa Mtaa wa Nsemulwa Migazini mjini humo ,kifungo cha miaka 20 jela kwa kosa la kutaka kumbaka mama yake mzazi.
Mwendesha Mashtaka Mkaguzi wa Polisi, Timoth Nyika, alidai mahakamani hapo kuwa mshitakiwa alitenda kosa hili Septemba 29, mwaka jana nyumbani kwa mama yake mzazi .
Ilidaiwa mahamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo Richard Kasele, ya kuwa siku hiyo mshitakiwa aliingia ndani ya nyumba ya mama yake na kisha kumshika kwa nguvu kwa lengo la kufanya naye mapenzi.
Kesi hiyo iliyovuta hisia za watu wengi mjini hapa ilidaiwa mahakamani hapo kuwa mama huyo licha ya kukataa kufanya mapenzi mwanae huyo bado aliendelea kumshika kwa nguvu na kumvua nguo mama yake huyo mzazi.
“Baada ya kuona hali hiyo mama huyo alipiga mayowe ya kuomba msaada Kwa majirani ambao walifika katika nyumba ya mama huyo na kumkuta mwanae akiwa amemlalia huku akiendelea kuomba msaada……..
‘Majirani hao waliweza kumwokoa mama huyo na kisha aliwapa maelezo ya kuwa mwanae alikuwa anamshika kwa nguvu na kumlazimisha wafanye nae mapenzi baada ya maelezo majirani waliamua kumkamata mthumiwa na kumpeleka katika Kituo cha Kati ch Polisi mjini humo ‘ alisema Nyika .
Hakimu Kasele alisema kuwa ameridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka kuwa pasipo kutia shaka yeyte kuwa mshtakiwa alitenda unyama huo ..
Baaada ya Hakimu Kasele kusikiliza pande hizo mbili za mashitaka ambapo u upande wa mashtaka ulileta mashahidi wawili miongoni mwao akiwa mama yake mzazi mabapo upande wa utetezi haukuwa na shahidi yeyote , alimtia mshitakiwa hatiani.
Mshitakiwa alipoombwa na mahakama hiyo ajitetee aliomba apunguzie adhabu kwani yeye bado nikijana hata hivyo ombi hilo lilipingwa vikali na mwendesha mashitaka kwa kile alichodai kama mshitakiwa aliweza kufanya nyama huo kwa mama yake mzazi kwa watu wengine itakuwa ni balaa .
Hakimu Kasele alisema Mahakama imemtia hatiani mtuhumiwa hivyo anahukumiwa kwa kosa la kuvunja sheria No. 158 (1.B) 3 ya marekebisho ya sheria ya mwaka 2002 ambapo adhabu yake ni kifungo cha miaka 20 jela, haa hivyo haikuwezakufahamika mara moja kama takata rufaa au laa.
Mwisho.
MAHAKAMANI ya Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Rukwa imemuhukumu Ernest Fredrick (38), mkazi wa Mtaa wa Nsemulwa Migazini mjini humo ,kifungo cha miaka 20 jela kwa kosa la kutaka kumbaka mama yake mzazi.
Mwendesha Mashtaka Mkaguzi wa Polisi, Timoth Nyika, alidai mahakamani hapo kuwa mshitakiwa alitenda kosa hili Septemba 29, mwaka jana nyumbani kwa mama yake mzazi .
Ilidaiwa mahamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo Richard Kasele, ya kuwa siku hiyo mshitakiwa aliingia ndani ya nyumba ya mama yake na kisha kumshika kwa nguvu kwa lengo la kufanya naye mapenzi.
Kesi hiyo iliyovuta hisia za watu wengi mjini hapa ilidaiwa mahakamani hapo kuwa mama huyo licha ya kukataa kufanya mapenzi mwanae huyo bado aliendelea kumshika kwa nguvu na kumvua nguo mama yake huyo mzazi.
“Baada ya kuona hali hiyo mama huyo alipiga mayowe ya kuomba msaada Kwa majirani ambao walifika katika nyumba ya mama huyo na kumkuta mwanae akiwa amemlalia huku akiendelea kuomba msaada……..
‘Majirani hao waliweza kumwokoa mama huyo na kisha aliwapa maelezo ya kuwa mwanae alikuwa anamshika kwa nguvu na kumlazimisha wafanye nae mapenzi baada ya maelezo majirani waliamua kumkamata mthumiwa na kumpeleka katika Kituo cha Kati ch Polisi mjini humo ‘ alisema Nyika .
Hakimu Kasele alisema kuwa ameridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka kuwa pasipo kutia shaka yeyte kuwa mshtakiwa alitenda unyama huo ..
Baaada ya Hakimu Kasele kusikiliza pande hizo mbili za mashitaka ambapo u upande wa mashtaka ulileta mashahidi wawili miongoni mwao akiwa mama yake mzazi mabapo upande wa utetezi haukuwa na shahidi yeyote , alimtia mshitakiwa hatiani.
Mshitakiwa alipoombwa na mahakama hiyo ajitetee aliomba apunguzie adhabu kwani yeye bado nikijana hata hivyo ombi hilo lilipingwa vikali na mwendesha mashitaka kwa kile alichodai kama mshitakiwa aliweza kufanya nyama huo kwa mama yake mzazi kwa watu wengine itakuwa ni balaa .
Hakimu Kasele alisema Mahakama imemtia hatiani mtuhumiwa hivyo anahukumiwa kwa kosa la kuvunja sheria No. 158 (1.B) 3 ya marekebisho ya sheria ya mwaka 2002 ambapo adhabu yake ni kifungo cha miaka 20 jela, haa hivyo haikuwezakufahamika mara moja kama takata rufaa au laa.
Mwisho.


No comments