Breaking News

MKUU WA MKOA KUPAMBANA NA WANAOHUJUMU UJENZI WA BARABARA ZA LAMI RUKWA

Mkuu wa mkoa wa Rukwa, Mhandisi Stella Manyanya.

MKUU   wa Mkoa  wa  Rukwa , Stella  Manyanya  ameonya kuwa  hatasita  kuwachukulia  hatua   za Kisheria

  wale   wote  wataobainika  kuhujumu  mradi   mkubwa  wa ujenzi  wa  barabara   ya Sumbawanga – Laela – Tuduma   kwa  kuiba  vifaa  vya  ujenzi  na mafuta  mali  ya   makumpuni   yanayojenga  barabra hiyo  kwa  kiwango   cha  lami .

Alisema  amelazimika   kutoa  onyo   hilo  katika kikao   kilichofanyika   jana  mjini  hapa  ambapo  kiliwajumuisha  vinogozi  waandamizi   wa  Serikali  mkoani  hapa ,  Wakandarasi   wa mradi  huo wa  barabara ,  wawakilishilishi  wa  Shirika za Changamoto  za  Milenia  (MCC-T)  wakiongozwa na   Mwakilishi  wa   Changamoto   za Milenia   kutoa  Washngton   DC , Jonathan  Saiger

Mkuu  huyo wa   Mkoa  pia  aliviagiza vyombo   vya  ulinzi  na  usalama mkoani   hapa  kuhakikisha  wahalifu  hao  wanakamatwa  na  kufikishwa  kwenye   vyombo   vya   haki  ili  sheria  ichukue  mkondo  wake .

Mhandishi  Mkazi  Paulo Grumette    kutoka  Kampuni  la Kihandisi  la  Egis  linalosimamisha mradi  huo  mkubwa  wa  barabara  alifichukuwa  kuwepo  kwa   genge  la kiharifu   ambalo  alidai  limesababisha  kupungua kwa  kazi   ya   ujenzi  wa  mradi  huo  kutokana   kufanya  wizi  mkubwa   wa  vifaa   vya  ujenzi   na mafuta

Alidai  kuwa  imebainika  kuwa  genge  hilo la  kihalifu   likifadhiliwa na  watu   wanaodaiwa kutoka Jijini  Dar Es Salaam  na Mji  wa Tuduma  ulipo   katika  mpaka  wa  nchi  jirni  ya  Zambia  umeweza  kuiba    nondo  zaidi ya  tani  300  na  saruji   zaidi  ya  tani  40  na   kuviuza  nchi  jirani   ya Zambia .

Alisema  kuwa genge hilo   la   kihalifu  linawahusisha   wakazi   wa maeneo  unapopita   mradi   huo   wa  barabara   kwa  kuwapa  ajira  ya  muda  ili  kuwasaidia   na  kufanikisha  wizi huo  mkubwa  ambao alidai   ni   vigumu   kufanywa  na wanavijiji pekee.

Kwa  upande wake, Mkuu  wa Mkoa  Manyanya   aliwahakikishia   wakandarasi   hao kuwa  Serikali  mkoa  kupitia    vyombo   vyake   vya  ulinzi  na  usalama  vinadhibiti   wizi  huo   ambao kwa   sasa  umefikia   hatua   ya  kutisha  ili   kuhakikisha   kuwa mradi  huo   una malizika  kama  ulivyopangwa .

“ Tumesikia  taarifa  za  wizi  huo   tena  wa  kiwango   kikubwa  sisi  kama  Serikali   nawahakikishia  kuwa  tutaudhibiti  ikiwa   ni  mchango  wetu   kwenu  kuhakikisha  kuwa  mradi   unakamilika  kwa  wakati  uliopangwa  pia   nachukua  nafasi  hii kuwaaagiza   watendaji wangu  watembelee  maeneo  hayo   na  kutoa  elimu  kwa   wananchi  kuhusu   umuhimu wa  mradi  huo “ alisem Manyanya .

Ujenzi  wa  barabara   ya  kutoka  Tunduma – Laela – Sumbawanga  yenye  urefu wa  kilomita 225  kwa kiwango   cha  lami  unafanya   na  makandarasi   watatu  tofauti  kutoka  China , Uturuki  na  Uholanzi  ambapo  lili  kuharakisha  ujenzi  wake  mradi  huo  umegawanya   katika   vipande  vitatu   vya Tunduma – Ikana , Ikana –Laela  na Lela  - Sumbawanga

 Mradi  huo   ambao  unatarajia kutumua  zadi  ya  Sh  bilioni 400  hadi  utakapo  kamilika   unafadhiliwa  na   Serikali  ya  Marekani   kupitia  Shirika  lake   la Changamoto  za  Milenia (MCC).

No comments