TRA RUKWA, YATOA MSAADA KWA WENYE MAHITAJI MBALIMBALI.
Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Rukwa, Augustino Mkandara. Picha kutoka Maktaba. habari zaidi soma hapo chini.
MAMLAKA Kodi ya Mapato nchini (TRA), mkoani Rukwa imetoa misaada wagonjwa waliolazwa hospitalini na kwa vituo vinanvyosaidia watoto yatima mkoani humo
Vituo viwili vinavyosaidia watoto yatima katika mjini wa Sumbawanga na kingine kilichopo katika kijiji cha kipande wilayani Nkasi, kwa pamoja vikiwa vinasaidia watoto zaidi ya sabini na wagonjwa wa hospitali ya mkoa na ile ya Dk. Atman zilizopo mijini humo. Walifaidika na misaada hiyo
Kampuni hiyo , TRA ilitoa misaada ya vyakula vikiwemo unga , mchele pamoaja na sabuni mafuta ya kupikia , premende na piskuti vyenye jumla ya zaidi ya Sh 640,000=.
Akizungumza kwa nyakati na maeneo tofauti wakati akitoa misaada hiyo Meneja wa Mamlaka Kodi ya Mapato mkoani humo , Agustino Mkandala alisema TRA imeamua kutoa misaada hiyo kama sehemu yake ya kujali jamii
“ TRA ni Mamlaka ambayo ina mikakati ya kusaidia jamii kila mwaka kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita ……. Ndio maana tumeamua kutoa misaada hii kwa vituo vinavyosaidia watoto yatima na wagonjwa mahospitalini
Huu ni utaratibu ambao TRA imejiwekea kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita ambao tunaenerdelea nao kila mwaka “ alisema Mkandala
Alifafanua kuwa mkakati huo wa kugawa misaada kwa makundi yenye mahitaji maalumu ni sehemu ya maadhimisho ya wiki mlipa kodi nchini ambapo inaadhimishwa nchini nzima na kilele chake kitakuwa Jumanne wiki ijayo .
Akizungumza wakati akipokea msaada hiyo kwa niaba ya wafanyakazi wa Hospitali ya Mkoa iliyopo mjini hapa Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, Dk Sharack Mtulla, alisema kuwa wamefarijika na msaada huo ambapo umekuja wakati muafaka na akashauri misaada ya jinsi hiyo iwe endelevu
“ Tumefarijika sana tunaomba misaada hii iwe endelevu kwetu ni sehemu ya tiba kwa wagonjwa wetu hapa pia naomba taasisi nyingine pia ziinge mfano wenu kwani kwa hakika mahitaji tulionayo katika kuwahudumiwa wagonjwa wetu ni mengi pekee yetu hatuwezi “ alisema Dk Mtulla
Mwisho
MAMLAKA Kodi ya Mapato nchini (TRA), mkoani Rukwa imetoa misaada wagonjwa waliolazwa hospitalini na kwa vituo vinanvyosaidia watoto yatima mkoani humo
Vituo viwili vinavyosaidia watoto yatima katika mjini wa Sumbawanga na kingine kilichopo katika kijiji cha kipande wilayani Nkasi, kwa pamoja vikiwa vinasaidia watoto zaidi ya sabini na wagonjwa wa hospitali ya mkoa na ile ya Dk. Atman zilizopo mijini humo. Walifaidika na misaada hiyo
Kampuni hiyo , TRA ilitoa misaada ya vyakula vikiwemo unga , mchele pamoaja na sabuni mafuta ya kupikia , premende na piskuti vyenye jumla ya zaidi ya Sh 640,000=.
Akizungumza kwa nyakati na maeneo tofauti wakati akitoa misaada hiyo Meneja wa Mamlaka Kodi ya Mapato mkoani humo , Agustino Mkandala alisema TRA imeamua kutoa misaada hiyo kama sehemu yake ya kujali jamii
“ TRA ni Mamlaka ambayo ina mikakati ya kusaidia jamii kila mwaka kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita ……. Ndio maana tumeamua kutoa misaada hii kwa vituo vinavyosaidia watoto yatima na wagonjwa mahospitalini
Huu ni utaratibu ambao TRA imejiwekea kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita ambao tunaenerdelea nao kila mwaka “ alisema Mkandala
Alifafanua kuwa mkakati huo wa kugawa misaada kwa makundi yenye mahitaji maalumu ni sehemu ya maadhimisho ya wiki mlipa kodi nchini ambapo inaadhimishwa nchini nzima na kilele chake kitakuwa Jumanne wiki ijayo .
Akizungumza wakati akipokea msaada hiyo kwa niaba ya wafanyakazi wa Hospitali ya Mkoa iliyopo mjini hapa Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, Dk Sharack Mtulla, alisema kuwa wamefarijika na msaada huo ambapo umekuja wakati muafaka na akashauri misaada ya jinsi hiyo iwe endelevu
“ Tumefarijika sana tunaomba misaada hii iwe endelevu kwetu ni sehemu ya tiba kwa wagonjwa wetu hapa pia naomba taasisi nyingine pia ziinge mfano wenu kwani kwa hakika mahitaji tulionayo katika kuwahudumiwa wagonjwa wetu ni mengi pekee yetu hatuwezi “ alisema Dk Mtulla
Mwisho


No comments