POLISI JAMII YAREJESHA NIDHAMU KWA WANAFUNZI WA SEKONDARI RUKWA
Jengo la polisi mkoa wa Rukwa. |
Wanafunzi hao ni wa shule za Sekondari za serikali za Kantalamba na Mafulala ambao walikuwa watoro kupindukia na kutumia muda wa vipindi vya darasani kunywa pombe za kienyeji aina ya ulanzi na kuvuta madawa ya kulevya aina ya bangi.
Mkuu wa kitengo cha Polisi jamii katika Jeshi la Polisi mkoa wa Rukwa, Sixmound Kibasa, alisema wakati akiwasilisha mada kwenye kikao cha wadau wa habari kilichofanyika kwenye ukumbi wa RDC iliopo jengo la mkuu wa mkoa wa Rukwa, Kikao hicho kiliandaliwa juzi na Klabu ya waandishi wa habari wa mkoa huo (RKPC).
Alisema kuwa baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema juu ya kuwapo kwa wanafunzi ambao wakitumia muda wa masomo kufanya vitendo hivyo viou sambamba na kunywa pombe walianza harakati za kuwatafuta na kuwapa somo la athari ya utoro, ulevi wa pombe na madawa ya kulevya.
"tuanzia Shule ya Sekondari ya wavulana ya Kantalamba tukawaeleza kwa lugha laini juu ya manufaa ya elimu kwao na kwa jamii nzima, athari za vilevi wanavyotumia.............
BAADHI ya watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu wakicheza kamali kwenye moja vichochoro vya mtaa wa maendeleo mjini Sumbawanga, muda ambao walitakiwa kuwa shuleni. |
No comments