Breaking News

WANAOHUJUMU MIRADI YA BARABARA RUKWA KUKIONA.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akiangalia kazi inayofanywa na kampuni ya Aasleff Bam International ya Uholanzi inayojenga barabara ya Laela - Sumbawanga kwa kiwango cha lami katika Mkoa huo jana.
  MKUU wa Mkoa wa Rukwa, Stella Manyanya  ameonya kuwa hatasita kuwachukulia hatua za  kisheria watakaobainika kuhujumu mradi mkubwa wa ujenzi wa barabara ya Sumbawanga – Laela  mpaka Tuduma kwa kuiba vifaa vya ujenzi.

Ametoa onyo hilo jana  alipotembelea  kambi   ya   Ujenzi  ya  Mkandarasi  Aarslef  iliyopo  kijijini   Ikanda  wilayani  Sumbawanga ambao  wanajenga  kipande  cha  barabara  kutoka  Laela  hadi  Sumbawanga  mjini   kwa kiwango   cha  lami .


Alisema  kuwa  amelazimika  kutoa  onyo  hilo kali  kufuatia   kwa  taarifa  ya  wizi  mkubwa  wa  vifaa   vya  ujenzi   vikiwemo  maelufu  ya  tani   ya  saruji , nondo na  maelfu  ya lita ya mafuta  hususani  mafuta ya  dizeli   vyote   vikiwa mali  ya   kampuni   hiyo  ya  ujenzi .



Pia aliviagiza vyombo vya ulinzi na usalama mkoani hapa kuhakikisha wahalifu hao wanakamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria ili sheria ichukue mkondo wake.


Meneja  wa Mradi   wa Kampuni  hiyo  ya  ujenzi ,  inayosimamia mradi huo, alidai kuna
genge la wahalifu ambalo alidai limesababisha kupungua kwa kasi ya ujenzi wa mradi huo kutokana kufanya wizi mkubwa wa vifaa vya ujenzi na  ambapo  zaidi ya  lita 30,000  za  mafuta  ya   dizeli  zimeripotiwa kuibiwa .

Hivi  karibuni  akihojiwa  na  gazeti hili  mjini  Sumbawanga  , Mhandishi Mkazi, Paulo Grumette kutoka Kampuni Egis inayosimamia mradi huo wa ujenzi  wa  barabara   ya   kutoka  Tunduma -  Laela  - Sumbawanga kwa kiwango   cha  lami , alikiri   kuwepo  kwa genge la wahalifu ambalo alidai limesababisha kupungua kwa kasi ya ujenzi wa mradi huo kutokana kufanya wizi mkubwa wa vifaa vya ujenzi na mafuta.


Alidai kuwa genge hilo linafadhiliwa na watu wanaodaiwa kutoka jijini Dar ss Salaam na katika  Mji wa Tuduma ulipo katika mpaka wa nchi jirani ya Zambia.


Kwa mujibu wa madai ya Grumette, genge limeshaiba nondo zaidi ya tani 300 na saruji zaidi ya tani 40 na kuviuza nchi jirani ya Zambia .

“Hali ni mbaya sana kwa kipande kile cha barabara kinachotoka Tunduma hadi Ikana, huko ndiko hujuma hiyo ya wizi mkubwa wa vifaa hivyo vya ujenzi na mafuta vinafanywa na

genge hilo la waahalifu,” alisema Grumette.

Alidai kwani eneo hilo limekubuhu kwa vitendo hivyo kwa kuwa ni rahisi kuvusha mali hiyo ya wizi na kuiuza nchi jirani ya Zambia.

 
 

 
Wakazi wa kijiji cha Msanzi wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa, wakiwa njia kuelekea nyumbani baada kutoka porini kutafuta ya kuni kwaajili ya matumizi yao.

No comments