Breaking News

WATUMISHI WA HOSPITALI YA MKOA WA RUKWA WAAGA MWAKA 2011, KARIBU MWAKA MPYA WA 2012



 Watumishi wa Hospitali ya mkoa walivyoaga mwaka 2011 na kukaribisha mwaka 2012 jana usiku mjini Sumbawanga.

WATUMISHI wa Hospitali ya mkoa iliyopo mjini Sumbawanga, wametakiwa kuacha tabia ya kupokea rushwa kutoka kwa wagonjwa kwani kufanya hivyo ni kujidhalilisha wao wenyewe na taaluma zao.

Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga, Abdul Maulid, alisema hayo jana wakati wa hafla ya kuuga mwaka jana 2011 na kuukaribisha mwaka mpya wa 2012, iliyofanyika katika ukumbi wa hospitali hiyo uliopo mjini hapa.


Alisema kuwa ni aibu na kujidhalilisha kwa watumishi hao kuomba rushwa kutoka kwa wagonjwa wanaofika hospilini hapo kwaajili ya kupata matibabu hali ambayo inasababisha wagonjwa hao kupoteza imani nao hivyo watumishi hao kudharaulika wao na taaluma zao katika jamii.


"nawasihi mfuate maadili ya kazi yenu.....msiwe walevi kupindukia na msipokee rushwa kutoka kwa wagonjwa kwani kufanya hivyo ni kujifedhehesha..... tuikatae rushwa, tena rushwa ndogo ndogo ni mbaya na udhalilishaji mkubwa kwa taaluma yenu" alisema Kaimu Mkurugenzi huyo ambaye alimwakilisha mkuu wa wilaya katika hafla hiyo.

Naye, Kaimu Mganga mkuu wa mkoa wa Rukwa, Dk. Shadrack Mtulla aliwapongeza watumishi wa hospitali hiyo kwa kufanya kazi kwa bidii na kadri ya uwezo wao licha ya kuwapo kwa changamoto nyingi ambazo zinawakabili ikiwamo ya kupokea malalamiko mengi kutoka kwa wagonjwa.

Muuguzi wa zamu katika hospitali ya mkoa iliyopo mjini Sumbawanga, Grece Kapyaka akipokea zawadi kwaajili ya kuwapatia wagonjwa kutoka kwa Samweli Mwangi ambaye ni Kiongozi Mkuu wa vijana wa kisabato wa kanisa la hilo lililopo kantalamba mjini hapa jana.
Baadhi ya vijana wa kanisa la waadvestista Wasabato la Kantalamba mjini Sumbawanga, wakitoa zawadi kwa mmoja wa wagonjwa waliolazwa katika hospitali ya mkoa mjini Sumbawanga jana.
WATANZANIA wametakiwa kujenga utamaduni wa kusaidia watu wenye mahitaji mbalimbali ili kuondoa dhana kwamba watu wa aina hiyo wametengwa na jamii.

Wito huo umetolewa jana na vijana wa Kanisa la Waadvestista Wasabato la Katantalamba wakati walipotembelea wagonjwa waliolazwa kwenye wodi za hospitali ya mkoa mjini Sumbawanga na kutoa zawadi mbalimbali sanjari na kuwaombea wapone haraka, kuwapongeza kwa kumaliza mwaka jana na kuwatakia heri ya mwaka mpya wa 2012.

Kwa mujibu wa kiongozi mkuu wa vijana hao wakisabato, Samweli Mwangi, zawadi ambazo wametoa ni mafuta ya kupakaa, dawa za miswaki, vitabu vya neno la mungu sambamba na sabuni za kuogea na kufulia vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya Sh 500,000.

Alisema kuwa jamii ya watanzania imekuwa haina utaratibu wa kuwatembelea na kuwasaidia watu wenye mahitaji mbalimbali ya hivyo watu hao kuona kama watengwa na sio sehemu ya jamii yetu kitu ambacho kinawafanya baadhi yao kukata tamaa ya maisha.


No comments