Breaking News

NURU TOGWA, KIJANA ALIYEKATWA MASIKO BAADA YA KUPITA KWENYE SHAMBA LA KANISA.

Kijana Nuru Togwa akionyesha jinsi alivyokatwa masikio yote mawili na walinzi wa mashamba ya Efatha Ministry  baada ya kunasawa akikatisha ndani ya mashamba hayo, kwa sasa ni hawezi kusikia vizuri tangu alipopata dhahama hiyo.

Na Mwandishi wetu

WASWAHILI usema hujafa hujaumbika.....wakimaanisha kwamba katika safari ya maisha lolote linaweza kutokea kwaama ya kwamba umezaliwa mzima wa viungo vyote lakini pasipo mategemeo unapata ulemavu.

Si kitu kigeni katika maisha ya siku hizi, lakini kuna mazingira  hata ukipata ulemavu wa kudumu inaweza isikuumize sana ila ikitokea unapata ulemavu katika mazingira ya uonevu, unyanyasaji na ukatili uliopindukia inaumiza sana.

Nuru Tongwa  miaka 30 ni m
moja wa wananchi  wa kijiji cha Malonje, ambaye kwa sasa  ni mlemavu, baada ya kukatwa masikio yote mawili kwa wakati mmoja kutokana na kile kilichodaiwa alipita ndani ya shamba la Mifugo la DAFCO- Malonje mkoani Rukwa.


Uchunguzi wa kina uliofanywa na mwandishi wa habari hizi  umebaini kuwa tangu Serikali ya mkoa wa Rukwa lilipouza shamba hilo lenye hekta 15,000  kwa gharama ya Sh milioni 600 kwa mwekezaji Nabii Josephat Mwingira wa Kanisa la Efatha Ministry, ukatili wa aina hiyo dhidi ya wananchi ni jambo la kawaida.

Kijana huyo kwa sasa ni mlemavu kwa kuwa hawezi kusikia vizuri tangu alipokatwa masikio yake, kwani unapozungumza naye inakulazimu utumie sauti ya juu sana ndio aweze kukusikia.

katika mahojiano na mwandishi wa makala hii, anasema kuwa "Muda mrefu kidogo umepita........ ni zaidi ya miaka mitano (5) tangu nilipokutana na ukatili huo ambao sitokuja kuusahau maishani mwangu......nilikuwa nikitoka Ziwa Rukwa,  ilikuwa ni asubuhi  na nilikuwa nimebeba kikapu cha samaki wabichi nikielekea mjini Sumbawanga.

Kuuza samaki hao maarufu kwa jina la hailali ambako ndiko kuna soko la bidhaa hiyo,  lakini nikiwa njiani kuelekea huko ghafla walitokea watu watano wakanisimamisha na kuniamuru nikae chini, na kunitaka kutoa maaelezo ya kwanini nimepita kwenye njia zilizopo shambani humo ili hali tayari kuna zuio?”.
 Kabla ya kueleza lolote nilianza kupata kipigo kutoka kwa wale watu ambao walikuwa ni walinzi  shamba la Malonje ambao walikuwa na silaha za jadi kisha kunichukua hadi kwenye kambi yao ambako nako niliendelea kupigwa.

Mwisho walinifunga kamba na miguu halafu walichukua panga na kunikata sikio la kwanza kisha kumalizia sikio la pili, hakika nilijisikia maumivu makali sana ambayo hayajawahi kutokea!, ambapo damu nyingi zilivuja na kupoteza fahamu ndipo nilifikishwa polisi kisha hospitali ya mkoa kwa matibabu, pasi kujitambua" alisema.

Togwa aliongeza kuwa baada ya kutoka hospitali aliwekwa rumande kwa kosa la kuiba ngano gunia 40 na siku iliyofuatwa alifikishwa mahakama ya mwanzo mjini Sumbawanga.

Ambako kesi hiyo ilitajwa mara moja tu lakini baada ya hapo iliharishwa kwa zaidi ya mara tisa kisha  hakimu akaniachia huru kwa kuwa  na upande wa walalamika kutoudhuria mahakamani.
Baada ya Kukatwa masiko.

Togwa alisema kuwa baada ya kukatwa masikio na kesi kutoendelea mahakamani, hakujua wapi atakwenda kudai haki yake hivyo alishawishika kuwafuata watu wa kitengo cha haki za binadamu mkoa wa Rukwa na kuwaeleza kile kilichomsibu, lakini nao walishindwa kumsaidia kwa namna yoyote ile.

Alisema kuwa mchumba wake aliyetarajia kumuoa jina linahifadhiwa kwa sasa, alimkataa na hadi sasa hajawahi kupata mchumba wala mwanamke wa kumuoa hivyo anahisi kuwa mnyonge na asiye na thamani tena ndani ya jamii.

Tongwa sasa ni mlemavu wa masikio, hajui akimbilie wapi ili asaidiwe kudai haki yake dhidi ya ukiukwaji huu a haki za binadamu.

Kijana Nuru Togwa (30) ambaye amekatwa masikio yake yote mawili, akiwa na mdogo wake aitwaye Sukuma Togwa nyumbani kwao katika kijiji cha Malonje nje kidogo ya Manispaa ya Sumbawanga.



No comments