Breaking News

VIONGOZI WA SACCOS RUKWA NA KATAVI WAPIGWA MSASA

Mkuu wa wilaya Mathew Sedoyeka akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa viongozi wa vyama akiba na mikopo (Saccos) yaliyoandaliwa na mradi wa hifadhi ya ziwa Tanganyika kwa ufadhili wa UNDP na GEF. Pembeni yake ni mratibu wa mradi huo, Hawa Msham.
Kutoka kulia ni Mkuu wa wilaya Mathew Sedoyeka, katika ni mratibu wa mradi wa hifadhi ya ziwa Tanganyika unaofadhiliwa na UNDP na GEF, Hawa Msham na kushoto ni Afisa Maliasili mkoa Nicholaus Mchome wakifuatilia mafunzo ya viongozi wa Saccos. 
Mratibu wa mradi wa hifadhi ya Tanganyika unaofadhiliwa na UNDP na GEP, Hawa Msham akitoa mada katika mafunzo kwa viongozi wa vyama vya akiba na mikopo kutoka mikoa ya Rukwa na Katavi yaliyofanyika katika ukumbi wa RDC mjini Sumbawanga. pembeni yake ni afisa maliasili Nicholaus Mchome. 
Baadhi ya washiriki wa mafunzo kwa viongozi wa vyama vya akiba na mikopo kutoka mikoa ya Rukwa na Katavi yaliyofanyika katika ukumbi wa RDC mjini Sumbawanga, wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zikiwasilishwa.

No comments