Breaking News

MWALIMU AUAWA KWA KUCHOMWA NA VISU MPANDA


MTU mmoja  aliyefahamika  kwa jina la  Mwita  Paulo (Ryoba) 25  mwalimu wa Shule ya Msingi Lukama Makazi ya Wakimbizi ya Katumba  Mkoa wa Katavi  ameuwawa  kikatili  kwa kuchomwa na  visu  kifuani na watu wasiojulikana

Tukio la mauaji hayo ya  kikatili dhidi ya mwalimu huyo  lilitokea hapo  juzi  majira saa mbili usiku  katika  eneo la  shule ya msingi  Mpanda  katika mtaa wa Mpanda Hotel  mjini hapa
 
Kamanda wa  Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi  Dhahiri Kidavashari  aliwaambia waandishi wa habari  kuwa   marehemu  kabla ya kifo chake hicho  aliaga kwenye  kituo chake cha kazi  katika shule ya Msingi Lukama  kuwa anakwenda mjini Mpanda  katika shule ya Sekondari ya Mwangaza kufanya mtihani wa  kidato cha sita

Alisema  marehemu  alikuwa amefuatana na waalimu  wenzake ambao wanafundisha shule  za msingi mbalimbali zilizoko kwenye makazi hayo ya Wakimbizi ya Katumba ambao nao walikuwa wanakwenda kufanya mtihani wa kidato cha sita kwenye kituo cha kufanyia mtihani   katika shule ya Sekondari ya Mwangaza

 Kidavashari   alieleza  marehemu akiwa na waalimu  hao  aliweza kufika katika shule ya mwangaza   na  kufanya mitihani yake  ambapo alikuwa akirudia kufanya mtihani ya  baadhi ya masomo  ambayo hakuwa amefanya  vizuri  katika masomo yake ya kumaliza kidato cha sita

Baada ya kumaliza mitihani walimu huyo na wenzake  walianza safari la kurejea kwenye vituo vyao vya kazi  katika makazi ya wakimbizi ya Katumba  lakini yeye aliamua kubaki mjini Mpanda

 Alisema  baada ya hapo marehemu  Paulo  hakuonekana  tena  mpaka mwili wake  ulipoonekana  katika  eneo la shule ya Msinngi Mpanda    mtaa wa Mpanda Hotel  huku ukiwa  amechomwa visu  katika sehemu zake za kifuani

No comments