Breaking News

Walimu waandamana Mpanda, Viongozi wakimbia ofisi zao

Walter Mguluchuma, Mpanda.

Hali haikuwa  shwari kwa zaidi ya saa moja kwenye Ofisi  za  Manispaa Halmashauri ya Mpanda,  jengo  ambalo linatumiwa pia na Mkuu wa Mkoa wa Katavi baada ya waalimu  zaidi ya 50 washule za Msingi  na  Sekondari wakiwa na viongozi kuandamana kwenda kwa mwajiri wao wakitaka  walipwe ya madai ya Sh milioni 120.

Tukio  hilo liltokea  jana  nyakati za saa nne asubuhi, hali ambayo ilisababisha  viongozi wa Manispaa hiyo kuweza kujifisha  huku walimu hao wakiimba nyimbo mbalimbali kwenye kolido za ofisi hizo kwa saa moja na zaidi.

Hali hiyo iliwalazimu viongozi wa mkoa na Manispaa hiyo kujitokeza na kufanya kikao cha dharula na walimu hao waliokuwa wameambatana na viongozi wa Chama cha walimu (CWT) wilaya na mkoa.

 Kaimu katibu  tawala  wa Mkoa  huo, Salumu  Shilingi ndiye aliyejitosa kusikiliza kilio hicho cha walimu, huku CWT wakiongozwa na katibu wa mkoa, John  Mshota  ambaye aliwasilisha  madai mbalimbali ya  walimu hao ambayo yamekuwa sugu.

Mshota  aliyataja  madai hayo  kuwa  kucheleweshewa  kurekebishiwa  mishahara,
kutolipwa  fedha  za nauli  za likizo  kuanzia  mwaka  2013 hadi  2015, kutolipwa  gharama za  masomoni, kutolipwa kwa walimu  wastaafu  za kuwarudisha  kwao,gharama za uhamisho na fedha za  matibabu.

Mwenyekiti  huyo wa  CWT  Mkoa wa  Katavi  alieleza  kuwa   mwajiri wao ambaye ni mkurugenzi wa   Manispaa  ya  Mpanda,  ameshindwa kupeleka  michango  wake  kwenye mfuko  wa PSPF  hali  ambayo    imewaathiri  walimu  wanaostaafu  kutolipwa malipo yao ya mafao ya kinunua mgongo  kidogo  na kutopewa  hati zao za malipo yao ya  msharahara Salary  Slips za  mwezi  Agosti 2008.

Alisema kutokana na madai hayo, ndio  maana  waliamua  kuandamana  hadi ofisini  kwa mwajiri  ili  waweze kupatiwa  majibu  ya  madai yao  wanayodai kwa muda mrefu  sasa  bila kuwepo   dalili za kulipwa  madai  hayo.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, ambaye ni Ofisa  Elimu  Sekondari,  
Enelia   Lungulu  alikiri  mbele ya  walimu hao kuwepo kwa madai hayo ya walimu.

Aliongeza kwamba tatizo la kutolipwa kwa walimu hao  halipo kwao  bali  tatizo la kucheleweshewa kwa malipo hayo lipo  hazina  ambayo  mpaka sasa hawazituma  fedha za madai ya walimu  kwenye  Manispaa hiyo na jitihada za mawasiliano  zinaendelea kufanyika.


2 comments:

  1. Serikali iwalipe walimu iache longolongo mbona madeni mengine inalipa kwanini walimu tu?.

    ReplyDelete
  2. Serikali iwalipe walimu iache longolongo mbona madeni mengine inalipa kwanini walimu tu?.

    ReplyDelete