Breaking News

Mwandishi RTD afariki dunia dunia na kuzikwa Katavi


Na Walter Mguluchuma, Katavi.

Mwandishi wa  zamani wa Radio  Tanzania (RTD) kabla ya kuwa shirika la Utangazaji (TBC) hivi sasa Lucas Matipa (77) amefariki  Dunia na kuzikwa huko wilayani Mpanda Mkoani Katavi.

 Kwa mujibu wa kaka wa marehemu Padri Somoni Matipa alisema Lucas  alifariki  hapo  jana  jioni nyakati za saa 12:30 nyumbani kwao maeneo ya mtaa wa  Majengo Manispaa ya Mpanda.


Padri Matipa alisema  marehemu  alizaliwa mwaka 1940 huko  katika Tarafa ya Karema wilaya ya Mpanda ambayo kwa sasa ni wilaya ya Tanganyika na alistaafu kazi ya uandishi wa Habari na utangazaji wa RadioTanzania mwaka 2006.

Inaelezwa kwamba enzi za uhai wake alifanya kazi kama mwandishi wa habari na mtangazaji wa RTD ambapo miongoni mwa aliofanya nao kazi ni marehemu David Wakati.

Alisema  marehemu   Lucas  Matipa  alianza  kusumbuliwa na  maradhi tangu mwaka juzi  hali  ambayo ilimlazimu atoke  Dar es salaam  alikokuwa  akiishi na  kurudi  nyumbani kwao Mpanda.

Ibada ya  maziko ilifanyika  jana  katika    kanisa   Katoliki  Jimbo la  Mpanda na  ibada  hiyo  iliongozwa na Paroko  Msaidizi wa  Kanisa  hilo  Padri  Dominick  Odiyambo  aliyesaidiana  na  Padri  Simoni  Matipa.

Wakati wa  misa  hiyo ya  mazishi   Padri  Odyambo  alieleza  kuwa  marehemu  Lucas  Matipa  wakati wa uhai wake  alifanya kazi  vizuri ya uandishi wa  habari na utangazaji  vizuri .

Alisema kutokana na utendaji wake  mzuri wa  kazi  ya uandishi wa  habari  ndio  maana taifa lilimwamini na yeye alibahatika   kuzungumza  nae mara  kwa  mara  katika  kipindi  cha  hivi  karibuni  na  alikuwa  akimwelezea  jinsi alivyofanya  kazi  ya  uhandishi wa  habati  hapa  nchini na  nje ya  nchi  kabla ya kustaafu  kwake  2006.

Mazishi ya  marehemu Lucas   Matipa  yalifanyika  jana  katika  makaburi ya Mwangaza na yalihudhuliwa na mamai ya  wakazi mji wa   Mpanda  na kuhudhuriwa  na  viongozi mbalimbali wa serikali. 

No comments